DALILI YA MPENZI ASIE
MWAMINIFU
Zifuatazo ni njia ambazo
ulaghai unatokea:
Fikiria kuwa hivi karibuni
umefunga ndoa na baada ya miezi miwili
mkeo anaondoka na kwenda kuhudhuria mazishi ya shangazi yake,
Jumamosi ifuatiayo uko nyumbani na kujiona mpweke sana na kuamua kwenda kwenye
majumba ya starehe na marafiki wa kazini kwako. Japokuwa ulikuwa hukupanga
unajikuta umekunywa pombe na kupata ujasiri wa kutongoza moja kati ya wasichana
uliowakuta huko. Japokuwa ni kweli unampenda sana mke wako siku hiyo unajikuta
unaondoka na dada alie mrembo zaidi ya mkeo na kumpeleka Gesti house. Siku
ifuatayo mkeo anakupigia simu na kuuliza akitaka kujua Jumamosi ilikwendaje
kwani amepewa habari kuwa hukuwepo nyumbani saa 3 za usiku. Kuna njia tatu za
kukabili swali hilo toka kwa mkeo.
(1) KUSEMA UKWELI
“Nilijisikia
upweke sana na nikaenda na George Boji na Amanda kwenye disco. Naona nilikunywa
kupita kiasi na nikavutiwa na demu moja na nikavunja amri ya sita, nikazini”.Hili
sio rahisi kutokea utajaribu kumueleza mkeo kuwa ulifuata sheria na kutozini na
kumbe ulizini.
(2) UONGO
KAMILI
Nilikaa nyumbani na kuangalia
TV hadi saa 2 na nikaenda kulala na sikusikia hodi yoyote.
(3) UKWELI USIO KAMILIKA
“Nilijisikia upweke na George
Boji aliponiomba niende nae Capri cabana nilienda
na kurudi saa sita. Hapa unasema ukweli lakini ukweli ambao haukukamilika,
unaondoa jambo kubwa katika maneno yako. Mkeo anaamua kuwa uliosema ni kweli
kumbe kuna jambo uliloficha. Japokuwa hakuna mtu anayestahili kudanganywa au
kulaghaiwa ni vyema kukumbuka kuwa kila
mtu anawajibika kuwa mkweli kabisa, Ni watu wa chache ambao wanaweza
kudhamiria kabisa kusema uongo na kuwaumiza wengine, watasema uongo au kutumia
ulaghai kwa sababu ni waoga au hawapendi malumbano na hivyo hutumia uongo kujiepusha.
Mwanaume au mwanamke anapoiba
mapenzi nje ya ndoa anazo sababu zake za kufanya hivyo na hawezi kukuambia
sababu hizo. Haileti raha Kufikiria juu ya watu wapendanano kusalitiana lakini
ukiwa mdadisi soma orodha ya mambo ambayo mwanaume au mwanamke angependa
kuficha kama siri ya moyoni mwake.
(1) MUDA
WA KUWA PAMOJA
Mtu atasema uongo na kutoa
sababu za uongo kuepuka kuwa pamoja na mwenziwe au kuonana nae. Mnaweza kuwa
mmekubaliana jumamosi mwende disco na mwenzio atakutumia ujumbe akikwambia kuwa
amepata wageni wa ghafla au anaenda kumuona shangazi mgojwa nk. Ataanza kuwa
hapati muda wa kukaa na kuongea na wewe. Huamka na kwenda kazini bila
mazungumzo ya kutosha. Akirudi toka kazini hakuna uchangamfu au mazungumzo
yenye maana.
(2) MAHUSIANO
YA NYUMA
Utaambiwa uongo juu ya marafiki
wa kike au wa kiume wa zamani tulikuwa marafiki tu wala hatujafanya mapenzi”. “Yule
alikuwa hafai, nakupenda wewe zaidi” nk.
(3) MIKUTANO
YA SIRI
Utadanganywa juu ya muda ambao
mwenzio alikuwa na mtu fulani, utaambiwa walikutana kwa bahati mbaya na
walikuwa hawakupanga kukutana au walikuwa na maongezi ya kikazi, au maandalizi
ya arusi n.k.
(4) MICHEZO AU UTANI NA WATU WA JINSIA TOFAUTI
Unapomkamata
akicheza au kutaniana na mtu mwingine wa
jinsia tofauti na yake atakuambia hakuna
lolote la kimapenzi. Katika uhusiano wao. Michezo au utani wa namna hii anakuwa
anao hata katika maongezi ya simuu.
(5) HISIA, MVUTO NA KUPENDEZWA
Utadanganywa
juu ya hisia zake juu ya mtu mwingine hasa wapenzi wa zamani au wafanyakazi
wengine, utaambiwa kuwa hakuna uhusiano wa kimapenzi. Uonapo hali ya uchangamfu
mkubwa anapokuwepo mtu wa jinsia tofauti na yake hapo inakubidi ufungue macho
sawasawa.
(6) TENDO LA NDOA
Utadanganywa kuwa wewe unajua
zaidi ya wengine, utasifiwa hata kama
hustahahili sifa. Tafuta ukweli halisi kadri mnavyoendelea katika mahusiano
yenu, iwapo sifa zitaendelea siku zote basi sifa hizo zitakuwa za kweli.
Utafiti uliofanyika na wataalamu wa sayansi ya mapenzi unaonesha karibu
asilimia 70 ya wanawake hujifanya wameridhisha kumbe hamna lolote.
(7) HISTORIA YA WAPENZI
Utadanganywa juu ya idadi ya
wapenzi waliokutangulia, vitu ambavyo alifanya na wapenzi hao wa zamani.
Ataanza kuwa na tabia ya kuongea na wapenzi wa zamani au kuzungumza juu yao. Kama
haachi kuzungumzia juu ya wapenzi wa zamani hiyo ni dalili mbaya katika
uhusiano wenu. Jiulize ni sababu gani inayomfanya akumbuke na kuanza
kuzungumzia wapenzi wa zamani? Kama ameanza
kukulinganisha na mpenzi wa zamani basi huenda ameanza pia kufikiria kukuacha
au kutokuwa mwaminifu.
Mwanzo wa dalili za wizi wa mapenzi
Kitakuwepo
kipindi Fulani ambapo mwenzio ataanzakuiba mapenzi na dalili ya haraka
kuonekana ni mabadiliko ya ghafla, mabadiliko kati ya jinsi ambavyo zamani
alikuwa akienenda na vile alivyo zoea kuenenda katika mahusiano yenu.
Mabadiliko ya ghafla siku zote yanasababishwa na kitu fulani kipya, uonapo hilo anza kufanya
uchunguzi. Kwa kuangalia yafuatayo:-
(1) Wezi wengi wa mapenzi huonyesha dalili ambazo hata wao wenyewe
hawawezi kujua na hivyo hawawezi kuzificha.
(2) Watu wengi hawaoni au kutoa tafsiri tofauti ya dalili za wizi
wa mapenzi japo kuwa ziko wazi kwa
kuwa hawazijui.
(3) Ukifahamu kitu cha
kutafuta unaweza kupata dalili nyingi
za wizi wa mapenzi kwa
kutumia macho yako, masikio yako na
ufahamu ulionao juu ya mpenzi wako.
(4) Sio dalili za wazi, ni dalili za ndanindani ambazo zinaweza
kabisa kumuumbua mwizi wa mapenzi.
(5) Ni vizuri zaidi uweze kuzigundua dalili za wizi wa mapenzi ili
kuokoa ndoa yako au uhusiano wako ukichelewa unaweza kuwa umechelewa kabisa na
uhusiano wako kufa.
Mpenzi
wako anapo kosa uaminifu inaumiza sana
na mara nyingi huleta chuki, mawazo mabaya juu ya mtu ambaye ulimpenda na kumwamini kabisa, Mwanamke au mwanaume anapoiba penzi
nje ya ndoa inakufanya uanze kujiuliza ni kitu gani ambacho mimi nimepungukiwa
hata mwenzangu aende kuiba penzi nje ya
uhusiano wetu? Unapata shida kutafuta ni kosa gani ulilofanya ambalo
limempa mwenzio sababu ya kukusaliti. Utajiuliza sasa nifanye nini?
Nafasi
za mtu kuweza kuvunja uaminifu ni nyingi mno hivyo usijidanganye kwa kufikiri
kuwa mke wako, mume wako kamwe hawezi kujaribiwa kufanya mapenzi na mtu
mwingine.Ni kweli kwamba wanaume ndio wanaongoza katika wizi wa mapenzi lakini
uchunguzi nilio fanya kwa miaka mitatu umenithibitishia kuwa wanawake nao hawako
mbali sana
kuwafikia wanaume. Hebu angalia jinsi idadi ya baa zenye Guest House na idadi
ya Guest House zinavyoongezeka kila kona ya mji. Nimeongea na madereva wa tax
na wao pia wamenithibitishia ya kwamba wanawake walioolewa nao wanajua kucheza
mchezo wa kuiba penzi nje ya ndoa. Katika uchunguzi wangu nimegundua kuwa
wanawake ni waangalifu sana
katika kuiba penzi kuliko wanaume
Ili
uweze kumkamata mwizi wa mapenzi huhitaji kwenda chuo cha polisi na upelelezi
na jarida hili limeandaliwa kukusaidia uweze kugundua dalili za mwizi mapema kabisa kabla
mambo hayaja fika mbali, uhai na uzuri wa ndoa yako unategemea sana
uwezo wako na maarifa ya kuweza kuzitambua dalili za mwizi wa penzi. Zifuatazo ni dalili
muhimu za kuangalia.
(1) KUJALI SANA JINSI
ANAVYOONEKANA
Mtu ambaye ameanza kuiba
mapenzi nje ya ndoa utamgundua kwa kurudisha tabia za mwanzoni mwa uhusiano
wenu. Ataanza kuvaa nguo za kupendeza zaidi kuliko ilivyokuwa kawaida ili kumvuta
vizuri mpenzi mpya, kama ni mwanamke utaona mitindo
ya nywele, perfume na upambaji ghafla umeongezeka nguvu na kasi. Angalia
mabadiliko haya katika nguo za kawaida hadi nguo za ndani. Kama
mabadiliko ya usafi na uvaaji yameanza ghafla basi huenda mabadiliko hayo sio
kwa ajili yako bali mpenzi mpya.
(2) JINSI ANAVYO KAA NA WEWE
Uhusiano wake na mpenzi mpya
utamfanya akuone wewe kuwa tishio la kufa kwa uhusiano huo wenye nguvu ya penzi
jipya linalong’ara. Anakuwa mwepesi sana
kukasirika, kugombana mara kwa mara. Hali hii ya kutoelewana anaifanya iwe
sababu ya kuhalalisha wizi wa penzi nje ya ndoa. Ataanza tabia za kutopenda
kwenda nawe katika maeneo ya starehe na kuwa na visingizio vya kumfanya asikae
nawe.
(3) ISHARA ZA MAZUNGUMZO
Vitu ambavyo mwenzio anachagua
au kukataa kuzungumzia ni ishara kuwa kuna jambo la kufichwa, katika
mazungumzo, anaweza kutaja majina ya watu wapya kwako, maeneo au hoteli mpya
ambazo wewe na yeye hamjawahi kwenda, maeneo na vitu ambavyo kwa kawaida alikuwa
akipenda kuzungumzia vinapotea katika mazungumzo yenu.
(4) TABIA ZA KIKAZI
Kazi za ofisini ni kisingizio
kikubwa kwa mwizi wa mapenzi, hii humpa muda wa kufanya madhambi yake na kuchelewa kurudi nyumbani ,au kutokaa
nyumbani, mara nyingi atakuwa anakwepa kukaa nyumbani kwa visingizio vya kuwa
na marafiki zake wa kazini. Atakuwa hapendi ufike kazini kwake kwa kuwa unaweza
kumkuta na mtu katika hali ambayo haionyeshi urafiki wa kawaida.
(5) ZAWADI
Kuwa macho kipindi cha siku za
wapendanao na sikukuu nyingine ambazo watu hupeana zawadi. Utaweza kugundua
kadi au zawadi zilizofichwa maeneo ambayo anadhani huwezi kugundua. Mara nyingi
zawadi hizo ni za wapenzi wake wa ziada. Pia uonapo unapewa zawadi za ghafla na
za thamani kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kwake kufanya basi zawadi hizo
lengo lake ni kukufumba macho, masikio na mdomo
pia. Lengo la zawadi hizi ni kukufanya uamini wewe uko peke yako na hivyo
kupuuzia dalili za wizi wake.
(6) TENDO LA NDOA
Kuwa macho uonapo kuwa mnafanya
tendo hilo mara chache kuliko kawaida na pia inawezekana ghafla ukaona mnafanya
tendo la ndoa mara nyingi zaidi kuliko kawaida, inapokuwa mara nyingi
inamaanisha kuwa wewe umekuwa uwanja wa mazoezi ili aweze kufanya vizuri zaidi
kwa mpenzi mpya, au mpenzi mpya ameweza kumrudhishia hamu ya tendo hilo na
hivyo anawatumia nyote wawili kama faida yake ili ajione kuwa yye ni mtemi.
(7) KUJIENGUA
Ataanza kuonyesha kutopenda
kuwa pamoja na familia yako au marafiki zako kwa hofu kuwa huenda wakawa
wamemuona katika maeneo mabaya na hivyo kukupa wewe taarifa. Anapata shida
kuonyesha kuwa anakupenda au kukujali mbele za ndugu zako au marafiki zako na
hivyo atatafuta sababu za kukwepa kuwa nao kwa muda mrefu. Na kama
akikubali atakuwa sio mchangamfu na huenda akasisitiza muondoke mapema.
(8) KUKWEPA MASWALI
Uonapo kuwa mwenzio anakwepa
kujibu maswali fulani ambayo ni rahisi sana
na ya kawaida fungua macho yako zaidi utaona makubwa au anaweza kujibu swali
rahisi baada ya kuulizwa mara ya pili jambo ambalo linaonyesha alikuwa
anatafuta uongo wa kukuambia. Anapoanza kusitasita kujibu maswali ambayo hapo
nyuma alijibu bila kusita jua mwizi anatafuta pa kujificha.
(9) HANA
MUDA WA KUWA NAWE
Anaweza kukwambia hana muda au
fedha ambazo mngeweza kutoka kwenda sehemu za burudani lakini rafiki yake
akimpigia simu haraka sana
atatoka. Na aondokapo atakwenda kwa muda mrefu na akirudi ukitaka maelezo
anakuwa mkali au anatoa maelezo mafupi sana.
Anaanza kuwa mchelewaji na ghafla anaweza kutoa sababu za kutaka atoke na muda
wa kurudi kwake huwezi kutabiri.
(10) MATUMIZI YA SIMU
Mwanaume au mwanamke ambaye ni
mwizi wa mapenzi anakuwa na mabadiliko ya wazi katika matumizi ya simu yake ya
mkononi. Utaona kwamba mara kadhaa
anashindwa kupokea simu na kuongea
mbele yako au anakuwa na wasiwasi mara simu ya mpenzi wake inapoingia, utaona kuwa simu yake
siku hizi haitoi mlio kabisa bali mitikisiko
(Vibrations), ukimpigia utaona inachukua muda mrefu kupokea simu kuliko kawaida au
unapomkosa na unajua ataona
MISSED CALL inachukua muda mrefu
kukupigia na kuuliza ulikuwa unahitaji
nini. Anapopokea simu ya mpenzi wake
na wewe uko nyumbani au karibu utamsikia akiongea kwa sauti ya chini
sana kuliko ilivyo kawaida, maongezi ya
minong’ono ni dalili kuwa kuna jambo la kuficha, kama
hakuna jambo la kuficha kwanini aongee kwa sauti ya chini
? Au kwa nini asikuruhusu ushike simu yake kama hana jambo
la kuficha? Anapokuwa anaongea na mpenzi wake mpya na wewe ukaingia ghafla utaona anakata simu haraka au anafupisha
maongezi na kuaga, unapouliza alikuwa anaongea na nani anakuwa mkali au
anaongea manenao ya kukwepesha au kuleta maongezi tofauti kabisa.Ukiwa
unaouwezo wa kushika simu yake na kuitumia basi kagua simu zilizopigwa katika
masaa ya ajabu au simu ambazo zilichukua muda mrefu katika maongezi, zifuatilie
namba hizo kwa makini, na uonapo zinarudiwa rudiwa basi anza kujua kwamba mwenzio huenda amepata
mpenzi mpya. Mwanamke au mwanaume anayeiba mapenzi atakuwa na tabia ya kufuta
rekodi zote za meseji (sms), namba alizozipiga au namba alizopokea, uonapo mara
nyingi simu yake iko tupu tambua ya kuwa kuna siri ambayo hataki kabisa wewe
uweze kuijua.
(11) RATIBA YA
KILA SIKU
Mwanamke
au mwanaume aliyeanza kuiba mapenzi ataanza kuulizia juu ya ratiba yako ya kila
siku.Atafanya hivyo ili aweze kumpangia mpenzi wake mpya ratiba ambayo
haitakupa wasiwasi, uonapo hili basigundua kwamba anakupa nafasi ya kumtega ili
uweze kumkamata.
UKAMATAJI WA MWIZI
FANYA KAZI
YA ZIADA: Weka rekodi ya kila kitu anachosema ambacho kinaleta
wasiwasi, weka rekodi ya siku, tarehe muda na mambo uyagunduayo. Tunza taarifa
hizi ili uweze kuwa na risasi za kutosha siku ya mapambano na mwizi huyu.
Itachukua muda lakini matokeo yake yatakufariji kuwa kazi yako haikuwa ya bure.
Zaidi ya yote taarifa nyingi hupata nguvu zaidi unapokuwa na taarifa nyingi za
zamani ambazo zinafanana na hizi mpya. Hakikisha kuwa mwenza hajui wala kuhisi
kuwa unamchunguza.
FUATILIA
MAMBO: Kama alisema
alichelewa sehemu fulani, ngojea
siku mbili zipite halafu muulize kuhusiana na
yale aliokueleza mwanzoni, ukiona maelezo yanatofautiana jua ulidanganywa, Uliza watu
aliokuwa nao, marafiki zake, kuwa mwangalifu
unapotaka maelezo, toka kwa
watu wengine, Ukiona marafiki
zake au wafanyakazi wenzake hawaelewi unachouliza andika hali hiyo ya wasiwasi kwa
kumbukumbu ya kukusaidia baadaye.
Usiwaamini marafiki zake mia
kwa mia, marafiki zake wanaweza kutumiwa kuwa ngome ya kuficha siri zake. Kwa mfano, anaposema alikuwa
mahali flani na rafiki yake ,tafuta muda ukiwa peke yako na mpigie simu huyo rafiki yake na
kumuuliza “Vipi ilikuwaje siku ile
walipoenda ZEZE HOTEL, walikuwa
wangapi, mambo yalikuwa shangwe au vipi?” kama marafiki
zake wanasita sita au wanakuwa wanaonekana kama hawajui la kusema jua
kuwa ulidanganywa.
KUAMINI NA HATARI ZAKE
Watu wengi wanapendelea sana
kuamini kuwa wake zao au waume zao hawawezi
kwenda nje ya ndoa au nje ya
uhusiano wao na hivyo kuamini kile kinachosemwa. Kumwamini mwenzio kunakufanya uwe na amani na
kunafariji pale usikiapo wake au waume
wa watu wengine sio waaminifu. Mara nyingi mtu anaweza kujitahidi sana kufumbia
macho dalili za wizi wa mapenzi kukwepa
maumivu ya kuuangalia ukweli ambao unauwezo wa kuleta maumivu, jambo
hili la kufumbia macho dalili za wizi
ndio sababu kubwa inayofanya mke au mume kuwa mtu wa mwisho kujua kuwa alikuwa anasalitiwa.
Mwizi wa mapenzi anatumia udhaifu kwa faida yake. Mwizi wa mapenzi
ata endelea kummweleza mpenzi wake mambo
ambayo anapenda kusikia (kamwe
mimi siwezi kufanya mapenzi na mtu
mwingine zaidi yako. Siku zote mwizi wa
mapenzi atakuwa anaangalia kama mwenzie
ameanza kuwa na mashaka na akigundua
kuwa ameanza kuwa na mashaka atabadilisha
mbinu zake za wizi ili kuepuka aibu ya kukamatwa. Unapotaka
kumkamata mwizi wa mapenzi jitahidi sana
asigundue kuwa unamuonea mashaka, jizuie, vumilia mpaka upate ushahidi kamili, ukikosea hapo
mwenzio ataanza kuwa mwangalifu zaidi
na itakuwa vigumu
zaidi kumkamata. Baada ya kusema
haya utaona kwamba yote yana hasara zake
kwa kuwa yana uwezo wa kumsaidia mwizi wa mapenzi,
hawezi kukubali kosa kabisa kama huna ushahidi wenye nguvu ya kutosha, mara nyingi hata ukiwa na ushahidi wa kutosha mwizi bado
atajitahidi kujitetea kuwa hana hatia.
NJIA ZA KUWEKA UKWELI WAZI
Kabla hujaweka mambo wazi ni
muhimu sana ufikirie juu ya
mabadiliko unayotaka yatokee katika
uhusiano wenu kuweka mabo wazi ni vigumu
kwa kuwa unafanya kitu ambacho mwenzio anakiona kama jambo linalomletea
aibu au fedheha. Ili kuweka uwazi vizuri bila matokeo mabaya fanya mambo
yafuatayo.
(I) CHAGUA MUDA NA SEHEMU
Fanya
jambo hilo mkiwa wawili peke yenu,
mahali ambapo mtu mwingine hawezi
kusikia mazungumzo yenu. Chagua muda ambao mwenzio hakuchoka, hana haraka na
ametulia, usifanye jambo hili wakati mwenzio anajiandaa kwenda kazini au safarini.
(II)
MUANDAE MWENZIO
Kabla ya kutoa au kueleza ushahidi wako mwambie
mwenzio kuwa kuna jambo muhimu ungependa kumshirikisha na muombe atulie na
asifanye au kusema kwa hasira.
(III)
ELEZEA KINAGANAGA
Jitahidi
kutoa maelezo yalio wazi na ya kutosha na epuka kutumia maneno
yenye sura ya hukumu au kulaumu.
Onyesha jinsi ushahidi wako ulivyo sababisha uone kuwa
hupendwi au umesalitiwa na kuumizwa. Jizuie usiongee kwa sauti kubwa au katika hasira ili
mwenzio asione kuwa anavamiwa na kushambuliwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni